Awe mwenye umri usiopungua miaka kumi na nane (18)
Awe mwenye tabia nzuri, mwaminifu na akili timamu
Awe amelipa Kiingilio, hisa na kuweka Akiba kwa kiwango kilichowekwa kwa mujibu wa Masharti haya na awe tayari kushiriki kikamilifu shughuli za Chama zinazompasa
Awe tayari kufuata Masharti ya Chama, Sheria ya Vyama vya Ushirika namba 6 ya mwaka 2013 na Kanuni zake wakati wowote
Maombi ya mwanachama yatafanywa kwa maandishi kwa Bodi ya Chama ambayo itayajadili na akikubaliwa atathibitishwa na Mkutano Mkuu
Maombi yakipokelewa ndani ya siku thelathini Bodi iwe imeshughulikia ombi/maombi na kutoa jibu kwa mwombaji au waombaji
Mwanachama atalipa kiingilio cha shilingi laki moja tu (100,000/=) na angalau Hisa tano au zaidi kati ya Hisa Hamsini (50) zenye thamani ya shilingi elfu Kumi (10,000/=) kila moja anazotakiwa kununua ndani ya miezi kumi na mbili tangu kujiunga na Chama
Kuchangia Akiba yake ya shilingi elfu Hamsini (50,000/=) au zaidi kila mwezi
Chama kitakuwa na daftari ya wanachama lenye maelezo muhimu ya kila mwanachama ambapo mwanachama ataweka saini yake